JINAMIZI LA PICHA CHAFU LAIANDAMA BONGO MOVIE, MSANII APATA AIBU BAADA YA PICHA ZAKE CHAFU KUVUJA MTANDAONI..!! NEY WA MITEGO AHUSISHWA JUU YA SAKATA HILI



Msanii wa Bongo Movies, Fatuma Ayubu ‘Bozi’ aliyewahi kuripotiwa kujiachia kimahaba na mwanamuziki Emmanuel Eribariki ‘Nay wa Mitego’ ametia aibu kubwa baada ya picha zake za utupu kuzagaa mitandaoni.


Kutokana na picha hizo ambazo zimeonekana kuzagaa katika mitandao mbalimbali na kuacha viulizo kwa wasanii wengi wanaomfahamu, mwandishi wetu alimtafuta Bozi ambaye alionekana kutafunatafuna maneno na kumtupia lawama nzito Nay wa Mitego ambaye aliwahi kumtumia picha hizo walipokuwa wapenzi.


“Mungu wangu sijui nitaweka wapi sura yangu, nilishtuka sana baada ya kuona picha hizo ni aibu kubwa kwangu, nashindwa hata kuelewa zimesambaa vipi maana hizi picha alikuwa nazo Nay, nilimtumia kabla hatujaachana sasa hata yeye namuuliza anasema eti hajazisambaza,” alisema msanii huyo.


TOA MAONI YAKO HAPO CHINI

0 comments: